JOHANNESBURG:Watoto laki moja huzaliwa wakiwa wana virusi vya HIV kila mwaka
10 Oktoba 2007Matangazo
Shirika la watoto la umoja wa mataifa UNICEF limesema takriban watoto laki moja nchini Afrika Kusini wanazaliwa wakiwa wameambukizwa virusi vya HIV na idadi nusu ya watoto hao hufariki kabla ya kufikisha umri wa miaka miwili.
Shirika la UNICEF katika ripoti yake limeeleza kuwa watoto wanaondelea kuishi hukabiliwa na maisha magumu katika jitihada za kuishi na ugonjwa wa UKIMWI.