EU kutoa msaada wa euro milioni 458 Mashariki ya Kati
16 Machi 2026
Kamishna wa usimamizi wa majanga wa Umoja huo, Hadja Lahbib, amesema hatua hiyo inaonesha ni kwa jinsi gani EU inaongeza juhudi zake kusaidia waathiriwa wa migogoro, wakati wadau wengine wakipunguza mchango wao.
Kati ya fedha hizo, euro milioni 210 zitatolewa kusaidia raia nchini Syria kwa mahitaji kama chakula, huduma za afya, makazi, maji safi na elimu kwa watoto waliokosa masomo. Takwimu za Umoja wa Ulaya zinaonyesha kuwa watu milioni 16.5 Syria wanahitaji msaada wa kibinadamu.
Aidha, euro milioni 124 zitatolewa kusaidia mahitaji ya msingi katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi, huku euro milioni 100 zikitengwa kwa msaada wa kibinadamu nchini Lebanon.
Fedha nyingine euro milioni 15.5 zitaelekezwa Jordan na euro milioni 8 nchini Misri kusaidia juhudi za misaada ya dharura.