1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Myanmar yakamilisha awamu ya mwisho ya uchaguzi mkuu

25 Januari 2026

Raia wa Myanmar wamepiga kura katika awamu ya tatu na ya mwisho ya uchaguzi mkuu nchini humo. Chama kinachoungwa mkono na jeshi kinatarajiwa kupata ushindi katika uchaguzi uliodumu kwa karibu mwezi mmoja.

https://p.dw.com/p/57PgJ
Mandalay. Myanmar 25.01.2026
Mkuu wa jeshi la Myanmar Min Aung Hlaing akitembelea kituo cha kura mjini MandalayPicha: Anthony Wallace/AFP

Chama hicho "The Union Solidarity and Development Party" (USDP) kilichosheheni maafisa wastaafu wa jeshi kilishinda kwa asilimia 85 katika uchaguzi wa baraza la wawakilishi na theluthi mbili katika bunge, kwenye awamu mbili za awali

Wakosoaji waulalamikia uchaguzi 

Wapiga kura kwenye miji 60 wanashiriki zoezi hilo katika miji mikubwa ikiwemo Yangon na Mandalay. Wakosoaji hata hivyo wanasema uchaguzi katika taifa hilo si huru wala wa haki na unalenga kuhalalisha mamlaka ya kijeshi ilisoiondoa serikali ya kiraia ya Aung San Suu Kyi Februari 2021.