Nchini Tanzania kumekuwa na hisia tofauti baada ya kuachiwa huru kwa mwanahabari wa upelelezi Erick Kabendera baada ya kukubali kulipa faini ya zaidi ya shilingi milioni 200 za Kitanzania. Shirika la haki za binaadamu la Amnesty International limeikaribisha hatua hiyo ya kuachiwa kwake. Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini humo - LHRC Bi Anna Henga alizungumza na Bruce Amani.