JangaVenezuela
Watu 32 wafariki Venezuela kufuatia tetemeko la ardhi
25 Juni 2026
Matangazo
Serikali imeonya kuwa idadi ya vifo na majeruhi inaweza kuongezeka kadri juhudi za uokoaji zinavyoendelea.
Hakukuwa na takwimu kamili kutoka jimbo la Guaira, eneo la pwani ya Bahari ya Karibi ambalo limeathirika vibaya zaidi.
Kiongozi huyo wa Venezuela amelieleza jimbo hilo kama "eneo la maafa", akisema matetemeko hayo ya ardhi yaliyotokea mfululizo ni janga la kitaifa, na serikali imetangaza hali ya hatari.
Wafanyakazi wa uokoaji wanaendelea kuwatafuta manusura wanaohofiwa kufunikwa chini ya vifusi vya majengo yaliyoporomoka.
Huduma za treni kote nchini humo zimesimamishwa, na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Caracas umefungwa kutokana na uharibifu mkubwa uliotokea.