Jijini Dar es salaam katika eneo la Namanga, ndipo kilipo kitovu cha biashara ya maua. Biashara hiyo inazidi kushika kasi ambapo maua yamekuwa na soko. Maua hutumika katika mapambo mbalimbali, kama vile harusi, mazishi, na sherehe nyingine. Hawa Bihoga anazungumza na wafanyabiashara wa kike kufahamu changamoto zilizopo katika makala ya Wanawake na maendeleo.