Wataalamu wa afya wameshauri kuwa njia moja muhimu ya kuepusha kusambaa kwa virusi vya corona ni kunawa mikono kwa sabuni na maji yanayotiririka. Ili kufanikisha hayo, kijana mmoja amebuni kifaa kinachosaidia katika unawishaji mikono bila ya kuwa katika hatari ya kuambukizwa virusi hivyo.