1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ulaya kuipatia Ukraine risasi milioni 1

Grace Kabogo
20 Machi 2023

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Ulaya wamekubaliana kuipatia Ukraine risasi milioni moja kwa ajili ya mifumo ya kurushia makombora katika kipindi cha miezi 12 ijayo.

https://p.dw.com/p/4OwrS
Ukraine Chasiv Yar | Stapel von Munition bei Artilleriestellung nahe Bachmut
Picha: Narciso Contreras/AA/picture alliance

Nchi hizo pia zitapeleka haraka Ukraine risasi kutoka kwenye akiba zao zilizopo. Ukraine imeuambia Umoja wa Ulaya kwamba inahitaji makombora 350,000 kwa mwezi ili kuyasaidia majeshi yake kuzuia mashambulizi ya Urusi.

Soma pia: Umoja wa Ulaya waahidi kusimama na Ukraine bila kuchoka

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Catherine Colonna amesisitiza haja ya kuisaidia Ukraine zaidi, haraka na sasa. Makubaliano hayo yamefikiwa kutokana na wasiwasi kwamba Ukraine inaweza ikawa na uhaba wa aina muhimu zaa risasi katika siku zijazo.