1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Ukraine, Qatar, UAE kushirikiana katika sekta ya ulinzi

28 Machi 2026

Ukraine imefanya makubaliano ya ushirikiano katika sekta ya ulinzi na mataifa ya Qatar na Umoja wa Falme za Kiarabu. Makubaliano hayo yamefanyika wakati wa ziara ya Rais wa Ukraine kwenye nchi hizo.

https://p.dw.com/p/5BJXb
Ukraine, Qatar na Falme za Kiarabu zimekubaliana kushirikiana katika sekta ya ulinzi
Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskyPicha: Ukrainian Presidential Press Service/AFP

Qatar na Ukraine zimetia saini makubaliano yanayohusisha ushirikiano katika kupambana na kitisho cha droni na makombora. Kwa upande wa Falme za Kiarabu Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema amekutana na Rais Mohamed bin Zayed Al Nahyan na kwamba wapo kwenye hatua za kukamilisha makubaliano. 

Iran yadai kushambulia kituo cha mifumo ya kupambana na droni ya Ukraine nchini UAE

Ameyasema hayo wakati Iran ikiarifu kuwa imekishambulia kituo cha Ukraine chenye mifumo ya kupambana na droni kilicho katika Falme za Kiarabu. Iran inadai kituo hicho kilitumiwa kuvisaidia vikosi vya Marekani kuishambulia. Hata hivyo Ukraine imekanusha taarifa ya kushambuliwa kwa kituo hicho na kusema madai ya Iran ni ya uongo.