1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroYemen

Ugiriki yajiunga na oparesheni ya ulinzi bahari ya Sham

27 Februari 2024

Meli ya kijeshi ya Ugiriki imeelekea katika bahari ya Sham kushiriki katika oparesheni ya kuzilinda meli dhidi ya mashambulizi ya waasi wa Kihouthi wanaoungwa mkono na Iran.

https://p.dw.com/p/4cv46
Meli ya kijeshi katika bahari ya Sham
Meli ya kijeshi katika bahari ya ShamPicha: Hauke-Christian Dittrich/dpa/picture alliance

Mapema jana, serikali ya Ugiriki iliidhinisha ushiriki wa nchi hiyo katika oparesheni ya ulinzi ya jeshi la wanamaji la Umoja wa Ulaya iliyopewa jina la Eunavfor Aspides katika bahari ya Sham.

Ugiriki imesema ni muhimu kujiunga na oparesheni hiyo kwa kuwa hujuma zinazofanywa na waasi wa Houthi zimevuruga biashara ya kimataifa.

Meli kadhaa za kibiashara za Ugiriki zimeshambuliwa katika bahari ya Sham tangu mwezi Novemba, na kuharibiwa japo hakuna ripoti zozote za vifo vilivyoripotiwa.

Meli nyingi sasa zimetafuta njia mbadala kufuatia mashambulizi ya Wahouthi ambao wanadhibiti sehemu kubwa ya Yemen na ambao wanasema, wanazishambulia meli hizo kama ishara ya kuonyesha mshikamano kwa Wapalestina.

Ufaransa, Italia na Ujerumani pia zinashiriki katika oparesheni hiyo ya ulinzi ya Umoja wa Ulaya katika bahari ya Sham.