Katika Kinagaubaga hii leo, Mohammed Abdul-Rahman amezungumza na mwanasheria Awadh Ali Said aliyekuwa mjumbe katika tume ya mabadiliko ya katiba ya jaji Joseph Warioba, na kwa mapana watajadili kilio cha mabadiliko ya katiba nchini Tanzania, wakati ambapo tayari rais John Magufuli amesema hatatoa fedha kwa ajili kuuendeleza mchakato huo wa katiba mpya.