Kivuko cha MV Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Kisiwa cha Ukara mkoani Mwanza na Bugorora katika Ziwa Victoria, kimezama leo mchana kikiwa na abiria ndani. Hadi sasa kiasi ya watu watano wamethibitishwa kufariki dunia. Grace Kabogo amezungumza na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe, Esther Chaula, ambaye anaelezea hasa kile kilichotokea.