Uhispania na Ugiriki zimekubali kuwachukua tena waomba hifadhi ambao tayari walikwisha sajiliwa katika nchi hizo lakini walikuwa wakizuiliwa mpakani mwa Austria na Ujerumani. Canada imetangaza kuongeza ushuru katika bidhaa za Marekani ikiwa ni hatua ya kulipa kisasi. Na viongozi wa Umoja wa Ulaya wakubaliana kurefusha vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Urusi kwa miezi sita.