1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa Leo XIV atoa ujumbe wa matumaini kwa Walebanon

1 Desemba 2025

Kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni Papa Leo XIV, ametoa wito wa amani na kuvumiliana kidini katika kanda ya mashariki ya kati ambayo imezongwa na machafuko.

https://p.dw.com/p/54Xpo
Lebanon, Harissa 2025 | Papa Leo XIV akutana na waumini huko Beirut
Papa Leo XIV akihutubia umati wa watu wakati wa mkutano na maaskofu na viongozi wengine wa dini huko Harissa Lebanon, kaskazini mashariki mwa mji mkuu Beirut, Desemba 1, 2025.Picha: Andreas Solaro/AFP/Getty Images

Wito wa Papa Leo unawalenga vijana ambao imani yao imedidimia katika taifa ambalo limezongwa na migogoro.

Maelfu ya Walebnon walijitokeza barabarani kumpokea Papa Leo licha ya mvua.

Baada ya kuwasili Lebanon akitokea Uturuki katika ziara yake ya kwanza kimataifa kama Papa, Leo aliomba katika kaburi la Mtakatifu Charbel Makhlouf, kiongozi wa kidini Lebanon aliyeheshimiwa na Wakristo na vilevile Waislamu.

Papa Leo anatarajiwa kukutana na viongozi wa kanisa la Katoliki nchini humo wakiwemo maaskofu na watawa kisha ataongoza mkutano wa Pamoja unaozileta dini mbalimbali pamoja na viongozi wa Kikristo na Kiislamu wa Lebanon mjini Beirut.