1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiAngola

Papa Leo XIV aongoza misa kubwa nchini Angola

20 Aprili 2026

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo XIV ameongoza misa kubwa siku ya Jumapili katika mji mkuu wa Angola, Luanda.

https://p.dw.com/p/5CSiu
Luanda |  Papa Leo XIV akihutubia huko Angola
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo XIV akihutubia AngolaPicha: Guglielmo Mangiapane/REUTERS

Papa Leo alitembelea pia eneo takatifu la Mama Muxima pembezoni mwa Mto Kwanza na alifanya ibada katika hekalu la Kikatoliki lililokuwa kitovu cha biashara ya watumwa wa Kiafrika wakati wa utawala wa wakoloni wa Ureno huku akikukumbuka "huzuni na mateso makubwa" ambayo Waangola walivumilia kwa karne nyingi.

Angola ni kituo cha tatu katika ziara ya Papa Leo barani Afrika . Baada ya Angola, anatazamiwa kuelekea  Guinea ya Ikweta atakapohitimisha ziara yake ya siku 10 itakayokamilika Aprili 23, 2026.