1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

"Naogopa kuishi nje ya kituo cha hifadhi"

Amina Abubakar5 Machi 2015

Mtoto Hassan Khamis ni miongoni mwa walemavu wa ngozi wanaohifadhiwa kwenye kituo cha Buhangija nchini Tanzania na sasa akiwa ameshakuwa mkubwa na kulazimika kutoka hapo, anasema hana uhakika wa maisha yake.

https://p.dw.com/p/1ElGv
Watu wenye ulemavu wa ngozi katika kijiji cha Ruyigi, Burundi.
Watu wenye ulemavu wa ngozi katika kijiji cha Ruyigi, Burundi.Picha: picture-alliance/ dpa

Katika mfululizo huu wa ripoti maalumu mwezi mzima kuangazia masaibu, changamoto na maisha wanayopitia watu wenye ulemavu wa ngozi, maarufu kama albino, ambao hivi karibuni wamekuwa wakilengwa na kushambuliwa nchini Tanzania kwa imani za kishirikina, hapa Idhaa ya Kiswahili ya DW inazungumza na kijana Hassani mwenye umri wa miaka 17 sasa na ambaye amehifadhiwa katika kituo cha Buhangija kinachowashughulikia watu wanaoishi na ulemavu wa ngozi mjini Shinyanga, Tanzania.

Kusikiliza mahojiano na kijana Hassani, tafadhali bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Mwandishi: Amina Abubakar
Mhariri: Mohammed Khelef