Baadhi ya vijana wamejikuta wakipoteza mwelekeo wa maisha kutokana na kuikosa elimu ya afya ya uzazi kutoka kwa watu wao wa karibu. Mila na tamaduni zinaonekana kuwapa kibali thabiti wazazi kuificha elimu ya afya ya uzazi kwa vijana wao, hatua ambayo baadhi ya vijana wamejikuta wakiingia katika mapenzi ambayo si salama, huku hatima ya elimu yao ikisalia mashakani.