Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Halihalisi Publishers, wamiliki wa gazeti maarufu la Mwanahalisi, Said Kubenea, amesema wanapanga kuishitaki Serikali kwa kuisababishia hasara ya bilioni 2.2 sambamba na kumshitaki binafsi aliyekuwa Naibu Waziri Wa Habari Anastazia Wambura kwa matumizi mabaya ya madaraka, kufuatia Makama Kuu Nchini Tanzania kuondoa amri yakufungiwa gazeti hilo kwa miezi 24.