Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania Kangi Lugola amemuonya leo anayejiita ''mwanaharakati huru'' nchini humo Cyprian Musiba, kuachana na kuchafua majina ya viongozi, akijaribu kujionesha kana kwamba anatumwa na serikali. Musiba kwa upande wake amesema hatoacha alichokiita ''kumsemea Rais John Magufuli'' na yuko tayari kukamatwa. Yusra Buwayhid amemhoji Gwandumi Mwakatobe kuhusiana na hili.