Jumuiya ya nchi zinazopakana na bahari ya Hindi wanakutana mjini Aachen hapa Ujerumani kujadili njia za kukabiliana na majanga hasa yanayotokea katika mwambao au ukanda wa bahari hiyo. Josephat Charo amezungumza na mwakilishi wa Tanzania Elisa Mugisha, Mrakibu Msaidizi wa jeshi la zimamoto na uokoaji na kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji, wa mkoa wa kizimamoto wa Ilala, Dar es Salaam.