SiasaKorea Kaskazini
Korea Kaskazini na Belarus zasaini mkataba wa ushirikiano
27 Machi 2026
Matangazo
Mkataba huo umesainiwa baada ya Kim Jong Un kumkaribisha kwa ukarimu Rais Alexander Lukashenko katika ziara yake ya kwanza nchini humo.
Kim na Lukashenko ambao walikutana mara ya mwisho huko China mwaka jana, wamesema katika hali ya sasa ambapo mataifa makubwa duniani yanapuuza na kukiuka waziwazi kanuni na sheria za kimataifa, ni lazima nchi huru zishirikiane kwa karibu zaidi ili kuimarisha juhudi zinazolenga kulinda uhuru na kuboresha ustawi wa raia wao.
Mbali na kuiunga mkono Urusi katika vita vyake dhidi ya Ukraine, mataifa hayo mawili yananakabiliwa pia na vikwazo vya nchi za Magharibi na yanashutumiwa kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.