Iran yasema mwandamanaji Erfan Soltani hajahukumiwa kifo
15 Januari 2026
Matangazo
Mahakama hiyo imesema Soltani hajahukumiwa kifo na ikiwa atapatikana na hatia, kulingana na sheria, adhabu, itakuwa kifungo gerezani kwasababu hukumu ya kifo haitumiki kwa mashtaka kama hayo.
Macho yote yalikuwa yameelekezwa kwa Soltani, anayeshikiliwa katika gereza la Karaj viungani mwa Tehran tangu kukamatwa kwake, na ambaye anakabiliwa na mashtaka ya propaganda dhidi ya mfumo wa Kiislamu wa Iran na kuendana kinyume na usalama wa taifa.
Hayo yanajiri saa chache kabla ya kufanyika kwa mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ulioitishwa na Marekani.