1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Eneo la Sahel barani Afrika ndio kitovu cha ugaidi duniani

20 Machi 2026

Eneo la Sahel barani Afrika kwa sasa ndio "kitovu cha ugaidi duniani." Ripoti ya Ugaidi Duniani ya mwaka 2025 imesema eneo hilo lilichangia karibu nusu ya vifo vyote vinavyohusiana na ugaidi kwa mwaka wa tatu mfululizo.

https://p.dw.com/p/5Ancw
Niger Niamey 2019 | Wanajeshi wa Niger waliuawa 2019 kwenye mashambulizi ya kigaidi
Wanajeshi wa Niger waliuawa 2019 kwenye mashambulizi ya kigaidiPicha: Ludovic Marin/AFP

Faharasa hiyo iliyoandaliwa na taasisi ya Taasisi ya Uchumi na Maswala ya Amani imeziorodhesha nchi 163 kwa muda wa miaka 13 kulingana na athari za "ugaidi" kwa kuzingatia viashiria kama vile idadi ya mashambulizi, vifo, majeruhi na mateka.

Ripoti hiyo inafafanua ugaidi kama "tishio la kimfumo au matumizi ya nguvu, yanayofanywa na watendajizopo madarakani."

Niger Arlit 2010 | eneo la uchimbaji madini ya Urani katika jangwa kaskazini mwa Niger
Watu saba walitekwa nyara, katika uvamizi kwenye mji wenye shughuli za uchimbaji madini ya Urani katika jangwa kaskazini mwa Niger.Picha: Issouf Sanogo/AFP/Getty Images

Mnamo 2024, zaidi ya nusu ya vifo 7,555 vilivyotokana na "ugaidi" duniani kote viliorodheshwa kutokea katika eneo la Sahel, kwenye ukanda wenye ukame unaoenea kandoni mwa ukingo wa Afrika kusini mwa jangwa la Sahara kutokea Bahari ya Atlantiki hadi kwenye Bahari Nyekundu.

Upi mwelekeo

Taasisi ya Uchumi na Maswala ya Amani yenye makao yake makuu nchini Australia imesema mwelekeo huo haukubadilika sana mwaka wa 2025. Ripoti hiyo imesema. "Kitovu cha ugaidi kimehama kutoka Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, hadi eneo la Sahel la Kusini mwa Jangwa la Sahara."

Hata hivyo, Nina Wilén ambaye ni mkuu wa Mpango wa Afrika katika Taasisi ya Egmont ya Mahusiano ya Kimataifa na mwandishi wa kitabu kuhusu kulilinda eneo la Sahel, kinachoitwa ‘Securitizing the Sahel' amesema ndio maana sio jambo la kushangaza kwa ripoti hiyo kuyahusisha mashambulizi mengi katika eneo la Sahel na makundi ya Jama'at Nusrat al-Islam wal-Muslimin (JNIM ) na lile linalojiita Dola la Kiislamu (IS). 

Burkina Faso ni nchi iliyoathiriwa zaidi duniani kwa miaka miwili mfululizo. Niger, imo katika nafasi ya tatu ikiwa na ongezeko la matukio ya "ugaidi" katika mwaka wa 2025.

Ghana Tarikom | Wakimbizi kutoka Burkina Faso
Wakimbizi kutoka Burkina Faso waliokimbilia GhanaPicha: Claudia Lacave/DW

Nigeria imepanda hadi nafasi ya nne kwenye orodha, huku watu 750 wakiuawa mwaka wa 2025, mauyji hayo yameongezeka kwa asilimia 46 kutoka mwaka uliotangulia.

Makundi hayo ya wapiganaji wenye misimamo mikali yanaendelea kukuza harakati zake hadi kwenye pwani za nchi za Afrika Magharibi, hasa Benin, ambayo imepanda hadi nafasi ya 19 kutoka nafasi ya 26 kwenye orodha ya "ugaidi" duniani kote.