SiasaIsrael
Cohen: Hatua za Israel ni sawa na 'utawala wa moja kwa moja'
10 Februari 2026
Matangazo
Cohen ameiambia Radio ya Jeshi la Israel, hatua hizo zinathibitisha kwa dhati kwamba hakutakuwa na taifa la Palestina.
Maoni ya Cohen yanafuatia matamshi kama hayo yaliyotolewa na wajumbe wengine wa serikali ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, akiwemo Waziri wa Fedha Bezalel Smotrich na Waziri wa Ulinzi Israel Katz, ambayo pia yanaondoa kabisa hata mamlaka kidogo aliyonayo Mamlaka ya Palestina na haijulikani ni kwa kiwango gani inaweza kuwapinga.
Wapalestina, nchi za Kiarabu na makundi ya haki za binadamu wameita hatua hizo zilizotangazwa Jumapili kuwa ni unyakuzi wa eneo hilo, linalokaliwa na Wapalestina wapatao milioni 3.4, wanaopigania taifa lao huko siku za usoni.