Bi Kidude: msanii mkongwe aliyechangia Taarab ya Zanzibar
Muziki
1 Mei 2019
Jina la Bi Kidude sio geni Afrika Mashariki. Msanii huyo mkongwe anaedhaniwa aliishi hadi umri wa miaka 100, alitoa mchango mkubwa visiwani Zanzibar katika kuziendeleza nyimbo za zamani za Taarab na ngoma ya jadi ya unyago. Kuna wanaotoa wito wa kumtengenezea makumbusho yake pekee, kuenzi mchango wake katika sanaa visiwani humo.