Zelensky na Starmer wahimiza uungwaji mkono zaidi Ukraine
18 Machi 2026
Matangazo
Katika mazugnumzo yake na waziri mkuu wa Uingereza mjini London, Zelensky amewataka washirika wa Ukraine kutoisahau nchi yake, na akapendekeza kwamba Marekani na mataifa mengine yatumie teknolojia ya Ukraine ya kupambana na droni katika vita vya Mashariki ya Kati ambavyo pia vimeufufua uchumi wa Urusi baada ya Marekani kuiondolea vikwazo vya mafuta yake kwa muda katika juhudi za kupunguza shinikizo kwenye usambazaji wa kimataifa uliosababishwa na vita katika Mashariki ya Kati.
Kwa upande wake, Starmer amesema haikubaliki kamwe Putin kuwa ndiye anayefaidika na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.