1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky na Starmer wahimiza uungwaji mkono zaidi Ukraine

18 Machi 2026

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy ameziita Urusi na Iran kuwa ni nchi "ndugu katika chuki" akitafuta kuungwa mkono na Waziri Mkuu wa Uimgereza Keir Starmer.

https://p.dw.com/p/5AayI
London 2026 | Starmer  katika mazungumzo na Zelensky afisini Downing Street
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky (kushoto) akizungumza na waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer wakati wa mkutano mjini London mnamo Machi 17, 2026Picha: Suzanne Plunkett/AFP

Katika mazugnumzo yake na waziri mkuu wa Uingereza mjini London, Zelensky amewataka washirika wa Ukraine kutoisahau nchi yake, na akapendekeza kwamba Marekani na mataifa mengine yatumie teknolojia ya Ukraine ya kupambana na droni katika vita vya Mashariki ya Kati ambavyo pia vimeufufua uchumi wa Urusi baada ya Marekani kuiondolea vikwazo vya mafuta yake kwa muda katika juhudi za kupunguza shinikizo kwenye usambazaji wa kimataifa uliosababishwa na vita katika Mashariki ya Kati.

Kwa upande wake, Starmer amesema haikubaliki kamwe Putin kuwa ndiye anayefaidika na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.