Zaidi ya raia 500 waliuawa kwenye mashambulizi Sudan
24 Machi 2026
Matangazo
Umoja wa Mataifa umesema hayo leo Jumanne na kuongeza kuwa mauaji mengi yalitokea katika jimbo la kimkakati la Kordofan.
Shirika la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa limesema kumekuwa na ongezeko kubwa la matumizi ya droni katika vita hivyo vya wenyewe kwa wenyewe vya Sudan.
Msemaji wa shirika hilo Marta Hurtado amewaambia waandishi Habari mjini Geneva kwamba katika wiki mbili za kwanza za Machi pekee, taarifa zilizopokelewa zinaonyesha kuwa zaidi ya raia 277 waliuawa. Zaidi ya robo tatu yao waliuawa katika mashambulizi ya droni.
Aliangazia hasa shambulio la tarehe 20 Machi dhidi ya Hospitali ya El-Daein, katika jimbo la Darfur Mashariki, lililoua watu 70, wakiwemo watoto 13, na kujeruhi wengine 146.