Sudan Kusini yadaiwa kuanzisha utawala wa kabila moja
12 Septemba 2025
Matangazo
Mashitaka dhidi ya Machar yalimfanya kiongozi huyo kuondolewa katika wadhifa wake.
Chama cha Machar cha SPLM-IO kilikanusha madai hayo pamoja na ya wanachama wengine 20. Madai yenyewe ni pamoja na mauaji, uhaini na uhalifu dhidi ya binaadamu. Chama hicho kimesema mashitaka hayo yamebuniwa na yamenuiwa kusambaratisha makubaliano ya amani.
Hatua ya Machar kuwekwa katika kizuizi cha nyumbani tangu mwezi Machi kimezua hofu ya kurejea kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe kama vile vilivyoshuhudiwa mwaka 2013 hadi 2018.
Vita hivyo vilisababishwa na mvutano kati ya makabila mawili yaliyotiifu kwa viongozi hao wawili, kabila la Nuer kutoka kwa Machar na Dinka kutoka kwa hasimu wake wa muda mrefu rais Salva Kiir.