1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIran

Trump na Starmer wazungumzia hali ya Mashariki ya Kati

16 Machi 2026

Rais wa Marekani Donald Trump amezungumza kwa simu na Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer kuhusiana na umuhimu wa kuufungua tena Mlango Bahari wa Hormuz, ambao kwa sasa umezuiwa na Iran.

https://p.dw.com/p/5ARb0
Uingereza USA 2026 | Rais Donald Trump wa Marekani na Waziri Mkuu wa Uingereza  Keir Starmer
Rais wa Marekani Donald Trump amezungumza na Waziri Mkuu wa Uingereza keir Starmer kuhusu hali kwenye eneo la Mashariki ya KatiPicha: DW

Ofisi ya Waziri Mkuu Starmer imesema viongozi hao walijadiliana kuhusu hali ilivyo Mashariki ya Kati pamoja na umuhimu kwa kufungua tena Mlango Bahari huo ili kukabiliana na kadhia ya usafirishaji na inayochochea kupanda kwa gharama kote ulimwenguni.

Trump, mapema aliyarai mataifa mengine kama China na Ufaransa kupeleka manowari za kivita kuisaidia Uingereza kuufungua mlango huo wa Hormuz

Starmer aidha alituma salamu za pole kwa familia za wanajeshi wa Marekani waliopoteza maisha kwenye vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran, imesema taarifa hiyo.