THE HAGUE:Charles Taylor afikishwa mahakamani
1 Juni 2007Matangazo
Rais wa zamani wa Liberia Charles taylor anafikishwa mahakamani siku ya jumatatu huko The Hague,Uholanzi.Kulingan na wa wataalam hatua hiyo inaashiria kumalizika kwa kipindi cha kuwaruhusu viongozi wa Kiafrika waliohusika na mauaji katili kuwa na uwezo wa kutoshtakiwa mahakamani.
Bwana Taylor anakabiliwa na mashtaka 11 ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sierra Leone.