Takaichi kuzungumza na Kim kuhusu utekaji wa raia wake
3 Novemba 2025
Matangazo
Takaichi amesema ili kujenga uhusiano ulio wa wazi na wakuaminiana, ni lazima akutane ana kwa ana na Kim Jong Un, kujadili suala hilo. Bado utawala wa Kim haujasema chochote kuhusu ombi hilo.
Viongozi wa zamani wamejaribu kuwa na mazungumzo na Kim kuhusu utekaji huo lakini juhudi zao hazikufua dafu.
Baada ya miaka mingi ya kukanusha madai hayo, mwaka 2002, Korea Kaskazini ilisema maafisa wake waliwateka nyara raia 13 wa Japan miaka ya 70 na 80, waliotumika kuwapa mafunzo ya lugha na tamaduni za kijapani wapelelezi wa Korea Kaskazini.
Hata hivyo Japan inaamini raia wake waliotekwa wanafikia 17 huku maafisa wengine wakisema idadi hiyo inaweza kuwa kubwa zaidi.