Migogoro
Taiwan yasisitiza ina haki ya kushirikiana na dunia
3 Mei 2026
Matangazo
Taiwan inadai kuwa China ilijaribu kuizuia. Akizungumza na Mfalme Mswati wa Tatu, Rais Lai alisema watu milioni 23 wa Taiwan wana haki ya kushiriki katika masuala ya kimataifa na kuchangia katika maendeleo ya dunia. Eswatini ni moja ya mataifa 12 pekee yenye uhusiano rasmi wa kidiplomasia na Taiwan.
China yaikosoa vikali ziara ya Lai
China imeikosoa vikali ziara hiyo, ikimtaja Lai kwa lugha kali, kauli ambayo Taiwan imeitaja kuwa isiyo na heshima na isiyofaa kidiplomasia. China inaichukulia Taiwan kama sehemu ya eneo lake na inapinga vikali uhusiano wowote wa kidiplomasia kati ya mataifa mengine na kisiwa hicho.