1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Utandawazi

WHO lahitaji dola bilioni 1 kushughulikia dharura duniani

3 Februari 2026

Shirika la Afya Duniani, WHO, limesema linahitaji kiasi cha dola bilioni moja mwaka huu kugharimia dharura za kiafya, magonjwa ya mlipuko na matibabu ya utapiamlo ulimwenguni.

https://p.dw.com/p/57zwR
Uswisi | WHO-Bendera ya WHO mbele ya makao makuu mjini Geneva wakati Marekani ikipunguza michango
Picha hii inaonyesha bendera ya Shirika la Afya Duniani (WHO) ikipeperuka katika makao yao makuu huko Geneva, mnamo Machi 13, 2025.Picha: Fabrice Coffrini/AFP


Mkurugenzi wa Mpango wa dharura za kiafya wa WHO, Chikwe Ihekweazu amesema mjini Geneva kuwa shirika hilo limezindua maombi ya michango na linatumai wachangiaji wapya na wa zamani kuongeza michango yao.

Takribani watu milioni 250 wanaishi katika maeneo yanaokabiliwa na mizozo ya kibinadamu duniani, bila usalama, mahali pa kulala wala upatikanaji wa huduma za afya, kulingana na Ihekweazu.

Hata hivyo kutokana na kupungua kwa bajeti, WHO hivi sasa inajikita tu kwenye mahitaji ya dharura, ikiwemo katika Ukanda wa Gaza, Mashariki ya Kati, Sudan, Ukraine, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Haiti na Myanmar.

Umoja wa Ulaya, Saudi Arabia, Ujerumani, Japan, Italia na Uingereza, ndio walichangia zaidi mwaka uliopita.