1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Ujerumani Steinmeier yuko ziarani Lebanon

16 Februari 2026

Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier anaanza hii leo ziara ya siku mbili nchini Lebanon.

https://p.dw.com/p/58q1F
Lebanon Baabda 2026 | Rais wa Shirikisho la Ujerumani Frank-Walter Steinmeier na Rais Joseph Aoun wakiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari
Rais wa Shirikisho la Ujerumani Frank-Walter Steinmeier amekwenda Lebanon kuonyesha mshikamano na taifa hilo katika harakati za kurejesha utulivuPicha: Mohamed Azakir/REUTERS

Steinmeier anatarajiwa kupokelewa na Rais Joseph Aoun mjini Beirut na atakutana pia kwa mazungumzo na Waziri Mkuu Nawaf Salam na spike wa Bunge Nabih Berri.

Siku ya Jumatano, Steinmeier ambaye anaambatana na mkewe Elke Büdenbender ataelekea Jordan.

Ofisi yake imesema ziara ya Steinmeier inalenga kupeleka ujumbe kwa mataifa hayo mawili ya Kiarabu kwamba Ujerumani inaendelea kuunga mkono juhudi za kurejesha utulivu