Papa leo awasili Angola kama sehemu ya ziara yake Afrika
18 Aprili 2026
Matangazo
Ndege ya kiongozi wa kanisa hilo ambaye ni wa kwanza kutokea Marekani, ilitua kwenye mji mkuu Luanda saa tisa alasiri.
Angola inakadiriwa kuwa na waumi milioni 15 wa kikatoliki ikiwa ni takriban asilimia 44 ya idiadi jumla ya watu nchini humo.
Papa Leo aliyeanzia ziara yake ya bara la Afrika nchini Algeria na Cameroon, anatarajiwa kukutana baadae na rais wa Angola Joao Lourenco kisha kutoa hotuba kwa umma.
Akizungumza na waandishi habari kabla ya kuanza safari yake ya Angola, Pape Leo XIV alisema anajutia matamshi yake ya kupinga vita duniani, kuchukuliwa kama ugomvi wa maneno na Rais wa Marekani Donald Trump, akisema hana muda wa kugombana na rais huyo.