1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa Leo akutana na viongozi wa Kikristo Mashariki ya Kati

28 Novemba 2025

Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo wa kumi na nne, amelaani ghasia zinazotokea kwa jina la dini wakati wa tukio la kihistoria na viongozi wa Kikristo kutoka Mashariki ya Kati.

https://p.dw.com/p/54S2g
Uturuki Istanbul 2025 | Paps Leo XIV.
Papa Leo (kulia) akutana na Rabbi David Sevi (kushoto) nchini Uturuki wakati wa ziara ya kwanza nje ya kidini nchini Uturuki mnamo Novemba 28, 2025Picha: Simone Risoluti/Vatican Media/REUTERS

Katika sherehe za maadhimisho ya miaka 1,700 ya baraza kuu la Kanisa lenye makasisi wakuu kutoka nchi zikiwemo Uturuki, Misri, Syria na Israel, zilizoandaliwa mjini Iznik ambao awali ulijulikana kama Nicaea, Papa Leo alisema ni kashfa kwamba Wakristo bilioni 2.6 duniani hawana umoja thabiti.

Kiongozi huyo wa kanisa Katoliki pia amesema kwasasa, ubinadamu wote ulioathirika kwa vurugu na mizozo unataka maridhiano na upatanisho.

Pia amesema lazima watu wapinge matumizi ya dini kuhalalisha vita, vurugu ama mfumo wowote wa kiitikadi na kuongeza kusema njia za kufuata ni mazungumzo na ushirikiano.