SiasaHungary
Orban aushutumu upinzani kutaka kunyakua madaraka kwa nguvu
10 Aprili 2026
Matangazo
Orban aliye madarakani kwa miaka 16, amedai kuwa wapinzani wanashirikiana na idara za ujasusi za kigeni kuwatishia wafuasi wake kwa vurugu huku wakilenga kunyakua madaraka kwa nguvu.
" Wanaanza kulalamika kuhusu udanganyifu kwa shutuma za uongo hata kabla ya uchaguzi. Wanaandaa maandamano na machafuko hata kabla ya kura zenu kuhesabiwa. Hebu tuzungumze wazi! Hili ni jaribio lililopangwa la kutilia shaka uamuzi wa watu wa Hungary kupitia machafuko, shinikizo, na shutuma za kimataifa," alisema Orban.
Kulingana na kura za maoni, Chama cha Fidesz chake Orban ambaye ni mshirika wa Urusi na Marekani, kinatazamiwa kushindwa na kile cha mpinzani wake Peter Magyar kinachounga mkono Umoja wa Ulaya.