Mwanadiplomasia mkuu wa Iran azungumza na Hamas
24 Juni 2026
Matangazo
Televisheni ya Iran imeripoti kuwa wakati wa mazungumzo hayo kwa njia ya simu, Araghchi alithibitisha tena uungaji mkono endelevu wa Iran kwa Wapalestina na harakati zao za haki hadi pale haki zao halali za kitaifa zitakapotekelezwa kikamilifu.
Mazungumzo hayo yanafanyika kufuatia kutiwa saini wiki iliyopita kwa hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani yenye lengo la kumaliza kabisa uhasama katika eneo la Mashariki ya Kati.
Hati hiyo haikutaja Gaza, lakini imeelezea kusitishwa mara moja na kukomeshwa kabisa kwa operesheni za kijeshi katika maeneo yote ya mapigano, ikiwemo Lebanon.