1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mwanadiplomasia mkuu wa Iran azungumza na Hamas

24 Juni 2026

Mwanadiplomasia mkuu wa Iran Abbas Araghchi, amezungumza na afisa mmoja mwandamizi wa tawi la kisiasa la Hamas Basem Naeem, kuhusu mazungumzo kati ya Iran na Marekani. Haya yameripotiwa leo na televisheni ya taifa.

https://p.dw.com/p/5Fy9U
Uswisi Geneva 2026 | Abbas Araghchi akihutubia mkutano wa Umoja wa Mataifa
Waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas AraghchiPicha: Jean Marc Ferré/MAXPPP/picture alliance

Televisheni ya Iran imeripoti kuwa wakati wa mazungumzo hayo kwa njia ya simu, Araghchi alithibitisha tena uungaji mkono endelevu wa Iran kwa Wapalestina na harakati zao za haki hadi pale haki zao halali za kitaifa zitakapotekelezwa kikamilifu.

Mazungumzo hayo yanafanyika kufuatia kutiwa saini wiki iliyopita kwa hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani yenye lengo la kumaliza kabisa uhasama katika eneo la Mashariki ya Kati.

Hati hiyo haikutaja Gaza, lakini imeelezea kusitishwa mara moja na kukomeshwa kabisa kwa operesheni za kijeshi katika maeneo yote ya mapigano, ikiwemo Lebanon.