1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Messi kuendelea kuichezea timu ya Marekani ya Inter Miami

18 Septemba 2025

Nyota wa kandanda na raia wa Argentina Lionel Messi anatarajiwa kuongeza mkataba wa miaka kadhaa na timu ya Marekani ya Inter Miami bila hata hivyo kutaja kitita cha mkataba huo.

https://p.dw.com/p/50eLC
Buenos Aires I Nyota wa kandanda na raia wa Argentina Lionel Messi
Nyota wa kandanda na raia wa Argentina Lionel Messi akiwa mjini Buenos Aires wakati wa mechi ya kufuzu kushiriki Kombe la Dunia mwaka 2026 kati ya Argentina na VenezuelaPicha: Gustavo Garello/AP Photo/picture alliance

Kulingana na taarifa iliyotolewa na kituo cha televisheni cha ESPN, pande zote ziko katika hatua za mwisho za mazungumzo, na kwamba ni mambo machache ambayo bado yanahitaji kukamilishwa.

Messi , mwenye umri wa miaka 38, alijiunga na Inter Miami katika msimu wa mwaka 2023 na mkataba wake ulikuwa unakamilika mwishoni mwa msimu huu.