1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tunisia yatakiwa kuimarisha uhuru wa kujieleza

18 Mei 2024

Makundi 10 ya kutetea haki za binaadamu yamesema katika mkutano wao wa pamoja mjini Tunis kwamba uhuru wa watu wa Tunisia unatishiwa chini ya uongozi wa rais Kais Saied

https://p.dw.com/p/4g1xa
Makundi ya kutetea haki za binaadamu yaitaka Tunisia kuimarisha uhuru wa kujieleza
Rais wa Tunisia Kais SaiedPicha: Chokri Mahjoub/ZUMA Wire/IMAGO

Mashirika hayo pia yamesema utawala unatumia mahakama na polisi kuwaadhibu wapinzani wao.

Mwezi huu pekee polisi iliwakamata watu 10 wakiwemo mawakili, wanaharakati, waandishi habari, na maafisa wa mashirika ya kiraia katika kile Amnesty Internationa na Human Rights Watch ilichokielezea kama kamata kamata dhidi ya wapinzani wa serikali. 

Amri dhidi ya "habari za uongo" inawakandamiza wakosoaji,Tunisia

Mashirika hayo yametoa wito kwa serikali ya Saied kuheshimu haki ya uhuru wa kujieleza ya watu wa Tunisia