1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Magazeti: kutano wa mazingira wa Umoja wa Mataifa waanza

Sekione Kitojo
4 Desemba 2018

Magazeti ya Ujerumani  yamejishughulisha zaidi na mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mazingira nchini Poland,  vita vya kibiashara kati ya  Marekani na China na maandamano  nchini  Ufaransa ya vizibao vya  njano.

https://p.dw.com/p/39Pz0
UN-Klimakonferenz 2018 in Katowice, Polen | Teilnehmer
Washiriki wa mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi Cop 24Picha: Getty Images/AFP/J. Skarzynski

 

Tukianza  na  gazeti  la  Badische Neueste Nachrichten  la  mjini Karlsruhe  mhariri  anazungumzia  kuhusu  mkutano  wa  mazingira , mhariri  anaandika:

Ilikuwa  ni  tone  tu  katika  bahari la  fadhaa, wakati  Marekani  chini ya  rais  wao  Donald  Trump  ambaye  ana  shaka  shaka na  suala la  mabadiliko  ya  tabia  nchi , alipoamua kujitoa  katika kufanyakazi kwa  pamoja  na  jamii  ya  kimataifa  kuokoa  sayari  yetu  ya  dunia dhidi  ya  uchafuzi wa  mazingira. Mtu  alifarijika  kwamba  mataifa mengine  kutokana  na  hali  hiyo  yanaweza  kufanyakazi  kwa pamoja. Muungano  wa wenye  busara  utazungumza  kwa  sauti moja  na uungwaji  mkono  dhaifu  wa  wale  ambao  wanaharibu mazingira  na  wasiojielewa, wangeondolewa  itakapofika  katikati  ya mwaka  2017. Kwa  bahati  mbaya  hayo  yalikuwa  ni matumaini  ya kupindukia, kama  inavyoonekana  hii  leo.

Ni  lazima  mkutano  huu  ulete  kitu muhimu,  na  kuondoka  katika hali  ya  kuhodhi  na  kujisikia  vizuri, na  kuendelea  na  mambo mengine , kwa  kuwanunua  wengine.  Anaandika  hivyo  mhariri  wa gazeti  la  Allgemeine Zeitung  la  mjini  Mainz  kuhusu  mkutano  huo wa  mabadiliko  ya  tabia  nchi. Mhariri  anaendelea:

Kwa  ukweli  kabisa , mtu  anaweza  kusema , hii  inaweza  kwenda kombo. Kwasababu  kimsingi ongezeko  la  ujoto  hususan lina  ncha nyingi. Mbali na  uzalishaji  mkubwa kutoka  mataifa  yenye  viwanda , lakini  pia  kuna suala  la ongezeko  kubwa  la  binadamu. 

Gazeti  la  Suedwest Presse  la  mjini  Ulm linazungumzia  kuhusu mada  ya  vita  vya  kibiashara  kati  ya  Marekani  na  China. Mhariri anaandika:

Sio Wajerumani  ama  Wachina  watakuwa  wanafurahia  matokeo ya  muda  mfupi  sana  ya  kuepuka   vita  vya  kibiashara  vya Marekani  ya  Donald Trump. Rais  huyo  wa  Marekani  atataka kuendeleza  mapambano  haya, na  kila  mara  atatafuta  njia  ya kuyaendeleza.

Nalo  gazeti  la  Suedkurie  linazungumzia  kuhusu vurugu zinazotokea nchini  Ufaransa, zinazofanywa  na  waandamanaji  wanaojiita wanaharakati  wa  vizibao vya  njano. Mhariri  anaandika:

Magari  yaliyochomwa  moto  pamoja  na  alama muhimu  katika eneo  maarufu  la  mjini  Paris  la  upinde  wa ushindi  iliyochafuliwa kwa  kuchorwa. Mwishoni  mwa  juma  wanaharakati  wa  vizibao vya  njano  walionekana  katika  mitaa mingi  ya  Ufaransa.  Hadi sasa  vuguvugu  hili  limekuwa  likipata  uungwaji  mkono  mkubwa. Lakini uharibifu  na  uchomaji  moto  mali  za  watu  haujasababisha wanasiasa  kuwekwa  kikaangoni. 

Ndani  ya  kundi  hilo  kuna  hali ya  ongezeko  la  nguvu , kama iliyotumika  katika  mkutano  wa  G20 mjini  Hamburg  na  kuharibu  mali  za  watu. Rais  anatumia  hali  hii ya  mabadiliko , anaweza  sasa kupambana  kuleta  utulivu, ambao Wafaransa  wanaupenda, wakati  wakiona  gari  inaungua  moto nje ya  nyumba.

Anatuma  polisi  katika  eneo  hilo, na  wanaopoteza katika  hali  hiyo  ni  wafuasi  wa  siasa  za  mrengo  wa  kushoto nchini  Ufaransa. Maandamano ya  kijamii  hayatayarishwi tena  na Wasoshalisti  ama  Wakomunisti, na  hata  pia  vyama  vya wafanyakazi. 

 

Mwandishi:  Sekione  Kitojo / inlandspresse

Mhariri: Iddi Ssessanga