Kura zaanza kuhesabiwa Benin baada ya uchaguzi wa rais
13 Aprili 2026
Ikiwa atatangazwa mshindi atamrithi Rais Patrice Talon ambaye amemaliza muda wake madarakani wa mihula miwili ya miaka mitano.
Wadagni ambaye ameungwa mkono pia na Rais Talon, anamwagiwa sifa kwa usimamizi mzuri wa uchumi katika kipindi cha muongo mmoja uliopita licha ya taifa hilo kukabiliwa na uhalifu wa makundi ya itikadi kali.
Mwanasiasa huyo anayeungwa mkono na vyama viwili tawala anakabiliwa na upinzani wa wastani kutoka kwa Paul Hounkpe, ambaye kampeni yake haikuwa na msisimko na alinusurika kukosa idadi inayohitajika ya udhamini ili kushiriki uchaguzi.
Mkuu wa Tume ya Uchaguzi ya Benin, Sacca Lafia, amesema uchaguzi ulifanyika kwa amani licha ya madai kadhaa madogo yaliyoripotiwa na asasi za kiraia. Matokeo ya awali ya uchaguzi huo yanatarajiwa baadaye wiki hii.