1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIsrael

Israel yapata mabaki ya mwisho yaliyozuiliwa Gaza

27 Januari 2026

Jeshi la Israel limethibitisha kupata mabaki ya mateka wa mwisho aliyebakia Gaza, hatua inayotimiza sharti muhimu la awamu ya kwanza ya mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kukomesha vita katika eneo hilo.

https://p.dw.com/p/57Yd9
Israel Tel Aviv 2026 | Maafisa wa polisi wakitoa heshima kwa mwili wa mateka wa mwisho wa Israel, Ran Gvili.
Maafisa wa polisi wakitoa heshima kwa mwili wa mateka wa mwisho wa Israel, Ran Gvili.Picha: Ilia Yefimovich/AFP

Kulingana na jeshi, mabaki hayo ni ya afisa polisi Rani Gvili aliyekuwa anazuiliwa Gaza kwa zaidi ya siku 840 na yatarejeshwa kwa ajili ya mazishi.

Kupatikana kwa mabaki hayo kunaweza kuchochea kufunguliwa upya kwa Kivuko cha Rafah kati ya Gaza na Misri, ambacho ni lango kuu la kutoka kwenye eneo hilo lililoloharibiwa, kwa kuzingatia ahadi za Israel.

Mabaki ya Gvili yalizuiliwa Gaza tangu alipouawa katika shambulizi la Hamas la Oktoba 27, 2023 kusini mwa Israel, lililochochea vita vya miaka miwili kwenye Ukanda wa Gaza.