1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Janga

Israel imethibitisha kuanza operesheni ya ardhini Lebanon

16 Machi 2026

Jeshi la Israel leo Jumatatu limethibitisha kuanza operesheni ya ardhini ya kijeshi ya muda, itakayolenga maeneo kadhaa Kusini mwa Lebanon huku Vita vya Mashariki ya Kati vikiendelea kutanuka.

https://p.dw.com/p/5AUzW
Israel Lebanon 2026 | Israel yaanza operesheni ya ardhini dhidi ya Hezbollah Lebanon
Israel imethibitisha kuanza operesheni ya ardhini Kusini mwa Lebanon Picha: Avi Ohayon/REUTERS

Msemaji wa jeshi la Israel la IDF Nadav Shoshani, amesema operesheni yao inawalenga wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran wa Hezbollah pamoja na miundombinu yao.

Operesheni hiyo pia inasemekana kuwa sehemu ya mpango mpana wa kuwalinda raia wa Kaskazini mwa Israel.

Jenerali Shoshani hakusema iwapo IDF itataka kudhibiti maeneo mapya huko.

Kundi la Hezbollah lilianzisha mashambulizi dhidi ya Israel Februari 28, kupinga mauaji ya Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei, yaliyotokea kufuatia mashambulizi ya Israel na Marekani dhidi ya Jamhuri hiyo ya kiislamu.