G7 kukutana Ufaransa kupunguza mvutano na Marekani
26 Machi 2026
Matangazo
Mkutano huo wa siku mbili wa G7 unaofanyika nje ya mji wa Paris, nchini Ufaransa, unakuja katika wakati ambapo Ikulu ya White House ikisema kuwa Rais Donald Trump yuko tayari kwa mashambulizi makali zaidi ikiwa Iran haitakubali makubaliano ya kumaliza vita vya Marekani na Israel dhidi yake.
Katika safari yake ya kwanza nje ya nchi tangu vita hivyo vilipoanza, waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio ataungana na wanadiplomasia wenzake wakuu kutoka Canada, Ujerumani, Italia, Ufaransa, Japan na Uingereza, lakini siku ya pili ya mkutano huo.