Chama Kikuu cha Upinzani nchini Tanzania CHADEMA ambacho hakikushiriki Uchaguzi Mkuu kimezungumzia jinsi kilivyoutazama uchaguzi huo na matukio yaliyofuatia. Hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa uongozi wa juu wa chama hicho kutoa kauli. Makamu Mwenyekiti wa chama hicho John Heche aliyeachiliwa jana kutoka rumande pamoja na mengine amezungumzia matukio ya vurugu na vifo jinsi yanatazamwa na CHADEMA.