1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Cape Verde na Misri zaitoa kimasomaso Afrika kombe la Dunia

16 Juni 2026

Katika michezo iliyochezwa hapo awali Cape Verde iliwashangaza wapenda kandanda duniani kwa kutoka sare ya bila kufungana dhidi ya mabingwa wa Ulaya Uhispania. Misri nao wametoka sare ya 1-1 dhidi ya Ubelgiji.

https://p.dw.com/p/5FTgn
Fußball-WM 2026 | Gruppenphase | Spanien vs. Kap Verde | Torwart Vozinha liegt verletzt am Boden
Kipa wa Cape Verde Vozinha Picha: Jacob Kupferman/AP Photo/picture alliance

Mechi za Kombe la Dunia 2026 zinaendelea kutimua vumbi katika viwanja mbalimbali. Mchezo uliomalizika muda mfupi kati ya Iran dhidi ya New Zealand umemalizika kwa sare ya 2-2.

Katika michezo iliyochezwa hapo awali Cape Verde iliwashangaza wapenda kandanda duniani kwa kutoka sare ya bila kufungana dhidi ya  mabingwa wa Ulaya Uhispania.

Katika mchezo golikipa wa Cape Verde Vozinha amezikonga nyoyo za watu kwa umahiri wake aliponyaka michomo ya Uhispania. Kipa huyo amepata zaidi ya wafuasi milioni nne mtandaoni baada tu ya mchezo huo.

Vigogo wa Afrika Misri nao wametoka sare ya 1-1 dhidi ya Ubelgiji.

Leo ni zamu ya Senegal dhidi ya Ufaransa huku Iraq wakiwa kibaruani na Norway.