Bodi ya amani ya Trump kuanzisha eneo la ''kibinadamu'' Gaza
8 Julai 2026
Matangazo
Afisa mmoja ameliambia shirika la habari la AFP kwamba eneo hilo linaweza kuwa "hatua ya kuanzia" kwa kamati ya wataalamu wa Kipalestina, ambayo imekusudiwa kusimamia shughuli za kila siku za utawala wa Gaza katika kipindi cha mpito kutoka vitani, kwa mujibu wa mpango wa vipengele 20 wa Trump.
Eneo hilo la majaribio, ambalo linapangwa kujengwa mjini Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza, litalindwa na vikosi vya kimataifa kutoka kundi la ISF, taasisi mpya inayofanya kazi chini ya Bodi ya Amani.
Kamati ya Kitaifa ya Usimamizi wa Gaza, ambayo ni kundi la wataalamu wa Kipalestina lililoanzishwa na Bodi hiyo ya Amani, itasimamia zoezi la kuwahakiki watu na kudhibiti uingiaji na utokaji katika eneo hilo, kwa usaidizi wa vikosi vya ISF.