1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Waziri mkuu wa Uhispania afanya ziara nchini China

13 Aprili 2026

Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sánchez yuko nchini China, hii ikiwa ziara yake ya nne katika kipindi cha takriban miaka mitatu nchini humo, .

https://p.dw.com/p/5C6Y2
China Peking 2026 | Pedro Sánchez
Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez akitoa hotuba nchini China mnamo Machi 13, 2026Picha: Borja Puig de la bellacasa/La Moncloa/AFP

Akizungumza katika Chuo Kikuu cha Tsinghua mjini Beijing leo, Sánchez aliitaka China kutekeleza jukumu kubwa kimataifa, siku moja kabla ya kukutana na rais wa nchini hiyo Xi Jinping.

Sanchez ameongeza kusema China inaweza kufanya mengi kwa mfano kutaka sheria ya kimataifa iheshimiwe pamoja na kusitisha vita nchini Lebanon, Iran, Gaza, Ukingo wa Magharibi na Ukraine.

Ziara yake inakuja katika wakati mgumu wa kisiasa na kijiografia ambapo viongozi wa Ulaya wanajaribu kushawishi kusitishwa kwa vita vya Marekani na Israel nchini Iran, huku mahusiano ya Uhispania na Marekani yakiwa yamedhoofishwa na kauli za Sánchez za kukosoa vita hivyo.