1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Watu 12 wauawa nchini Ukraine kufuatia mashambulizi ya Urusi

8 Machi 2026

Watu 12 wakiwemo wanawake na watoto wameuawa usiku wa Jumamosi, wengine 16 wakijeruhiwa kufuatia mashambulizi ya makombora na droni ya Urusi katika miji mbalimbali ya Ukraine ikiwa ni pamoja na Kyiv, Odessa na Kharkiv.

https://p.dw.com/p/5A0QP
Kharkiv | Uharibifu mkubwa kutokana na mashambulizi ya Urusi
Uharibifu mkubwa kutokana na mashambulizi ya Urusi huko Kharkiv, Ukraine ambapo watu kadhaa wameuawa.Picha: Viacheslav Madiievskyi/NurPhoto/IMAGO

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amelaani mashambulizi hayo akisema Moscow haijaachana na nia yake ya kuisambaratisha Ukraine, huku akitoa wito wa kuwepo jibu la kimataifa akisema Urusi inaendelea kulenga makazi ya raia  pamoja na miundombinu ya nishati.

Zelensky amesema pia kuwa amezungumza hapo jana na Mfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman kuhusu hali inayoendelea Mashariki ya Kati na akapendekeza kutoa msaada wake wa kitaalamu wa namna ya kukabiliana na droni za Iran za Shaheed ikiwa nchi yake pia itaahidiwa msaada kukabiliana na Urusi. Mapema wiki hii, Zelensky alizungumza pia na viongozi wa Bahrain, Jordan, Kuwait, Qatar na Umoja wa Falme za Kiarabu.